Kijana aliyegeuza taka za plastiki kuwa malighafi Tanzania
Akiwa na umri mdogo tu chini ya miaka 17, Edgar Edmund Tarimo ameweza kubuni na kutengeneza mashine ya kutengenezea vigae vya sakafu, (Paving Blocks), kwa kutumia taka za plastiki na mchanga.
Kupitia ubunifu wake huo, ameweza kupunguza kiasi kikubwa cha taka za plastiki mitaani na kusaidia kupunguza uchafuzi wa mazingira zinazotokana na taka hizo.
Na Kupitia kampuni yake ya Green Venture tayari ameajiri wafanyakazi sita na kuweza kutoa kipato kwa takriban watu themanini, ambao hufanya kazi ya kumkusanyia taka za plastiki.
Edgar anasema alianza ujasiriamali akiwa na mtaji wa shilingi za Kitanzania elfu 40, na tayari ameweza kushika mpaka kiasi cha milioni nne za Kitanzania.



No comments